Juu ya mulima unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema, Solomono alijenga pahali pa kumutambikia Kemosi, mungu wa chukizo wa Wamoabu, na nafasi ya kumutambikia Milkomu, mungu wa chukizo wa Waamoni.
Si Solomono alitenda zambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Yeye alikuwa mufalme mukubwa kuliko wafalme wa mataifa mengine. Mungu akamupenda na akamufanya kuwa mufalme juu ya watu wote wa Israeli, hata hivyo wanawake wa mataifa mengine, wakamusukuma kutenda zambi.