Nitafanya hivyo kwa sababu Solomono ameniacha, akaabudu miungu ya kigeni: Astaroti mungu wa Wasidoni, Kemosi mungu wa Wamoabu, na Milkomu mungu wa Waamoni. Solomono ameniasi, ametenda maovu mbele yangu. Hakutii masharti yangu na maagizo yangu kama Daudi baba yake alivyofanya.
Juu ya mulima unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema, Solomono alijenga pahali pa kumutambikia Kemosi, mungu wa chukizo wa Wamoabu, na nafasi ya kumutambikia Milkomu, mungu wa chukizo wa Waamoni.
Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,
Lakini kwa sababu mutumishi wangu Kalebu ni tofauti, na amenitii kwa ukamilifu, nitamufikisha kwenye inchi hiyo aliyoingia ndani yake na wazao wake watairizi.
Kwa hiyo, muji wa Hebroni ni sehemu yao wazao wa Kalebu mwana wa Yefune Mukenizi mpaka hivi leo, kwa sababu Kalebu alikuwa mwaminifu kwa Yawe, Mungu wa Israeli.