Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 11:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 11:4
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

ni kusema wanawake wa mataifa ambayo Yawe alikuwa amewakataza Waisraeli akisema: “Musioe kwao wala wao wasioe kwenu kwa sababu wanawake hao watapotosha mioyo yenu kusudi muitumikie miungu yao.” Solomono aliwapenda sana wanawake hao.


Nitafanya hivyo kwa sababu Solomono ameniacha, akaabudu miungu ya kigeni: Astaroti mungu wa Wasidoni, Kemosi mungu wa Wamoabu, na Milkomu mungu wa Waamoni. Solomono ameniasi, ametenda maovu mbele yangu. Hakutii masharti yangu na maagizo yangu kama Daudi baba yake alivyofanya.


Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.


Kwa muda wa miaka makumi ine, Solomono aliitawala inchi yote ya Israeli, makao yake yakiwa Yerusalema.


Hivyo, Solomono alitenda maovu mbele ya Yawe, wala hakufuata kwa ukamilifu mapenzi ya Yawe kama baba yake Daudi alivyokuwa amefanya.


Basi, Yawe alimukasirikia Solomono, kwa sababu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa Israeli, ingawa yeye alikuwa amemutokea mara mbili


Rehoboamu mwana wa Solomono alikuwa na umri wa miaka makumi ine na mumoja alipoanza kutawala inchi ya Yuda. Naye alitawala kwa muda wa miaka kumi na saba katika Yerusalema, muji ambao Yawe aliuchagua kati ya miji ya makabila yote ya Israeli kusudi aabudiwe humo. Mama ya Rehoboamu jina lake lilikuwa Nama kutoka kabila la Waamoni.


Lakini nafasi ya kutambikia miungu juu ya vilima haikuharibiwa. Hata hivyo, yeye alikuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe maisha yake yote.


Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.


Solomono alimupenda Yawe, akashika masharti ya baba yake Daudi; lakini tu, naye alitoa sadaka na kufukiza ubani juu ya vilima.


Solomono alianza kujenga nyumba ya Yawe katika mwaka wa mia ine na makumi nane kisha Waisraeli kutoka Misri. Huo ulikuwa mwaka wa ine wa utawala wa Solomono juu ya Israeli, katika mwezi wa Zivu, ni kusema mwezi wa pili.


Nanyi, mukuwe waaminifu kwa Yawe, Mungu wetu, mukifuata masharti yake na kutii amri zake zote kama munavyofanya hivi leo.”


Kisha miaka makumi mbili ambayo Solomono alipitisha kwa kuzijenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme,


Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,


“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Umujalie Solomono mwana wangu kusudi kwa moyo wote ashike amri zako, ushuhuda na maagizo yako, atimize yote na apate kujenga nyumba hii ya utukufu niliyoifanyia matayarisho.”


Yawe alikuwa pamoja na Yosafati kwa sababu alifuata njia za kwanza za babu yake Daudi, wala hakumwabudu mungu Bali.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe ingawa hakutenda kwa moyo mukamilifu.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata njia za Daudi babu yake, na kushika amri za Yawe kwa uangalifu.


Wala asijipatie wake wengi; kama sivyo moyo wake utaasi. Wala asijipatie feza na zahabu kwa wingi sana.


Mukifanya hivyo wao watawapotosha watoto wenu wasimufuate Yawe, na kuwafanya waabudu miungu mingine, nayo hasira ya Yawe itawaka juu yenu, halafu atawaangamiza mara moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ