1 Wafalme 11:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20024 Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.
Rehoboamu mwana wa Solomono alikuwa na umri wa miaka makumi ine na mumoja alipoanza kutawala inchi ya Yuda. Naye alitawala kwa muda wa miaka kumi na saba katika Yerusalema, muji ambao Yawe aliuchagua kati ya miji ya makabila yote ya Israeli kusudi aabudiwe humo. Mama ya Rehoboamu jina lake lilikuwa Nama kutoka kabila la Waamoni.