Rehoboamu alioa wake kumi na wanane na wahabara makumi sita, akazaa wana makumi mbili na wane na wabinti makumi sita. Kati ya wake zake wote na wahabara wake, alimupenda zaidi Maka binti ya Abusaloma.
Leo hii, wanawake wa Persia na Media ambao wamesikia jinsi malkia Vashiti alivyofanya, watakuwa wanawaelezea viongozi wako; hivyo mazarau na chuki vitajaa kila pahali.
Niliendelea kutafuta mambo hayo, lakini sikupata. Kati ya wanaume elfu moja, nilipata kuona mwanaume mumoja anayestahili heshima, lakini kati ya wanawake wote, sikuona hata mumoja anayestahili heshima.
Hakuna anayekuwa sawa njiwa yangu. Anaenea kabisa. Ni kipenzi cha mama yake, ni binti wake pekee. Wabinti wanamwangalia na kumwita mwenye heri, nao malkia na wahabara wanaimba sifa zake.
Akafuatana nao kwenda Ofura kwa baba yake naye akawaua wandugu zake wote makumi saba juu ya jiwe moja. Lakini Yotamu, mwana mudogo wa Yerubali aliponyoka kufa, maana alijificha.