Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 ni kusema wanawake wa mataifa ambayo Yawe alikuwa amewakataza Waisraeli akisema: “Musioe kwao wala wao wasioe kwenu kwa sababu wanawake hao watapotosha mioyo yenu kusudi muitumikie miungu yao.” Solomono aliwapenda sana wanawake hao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 11:2
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ndiyo maana mwanaume anamwacha baba yake na mama yake, na kuambatana na muke wake, nao wawili wanakuwa mwili mumoja.


Lakini Sekemu akavutiwa sana na yule binti, akamupenda hata akaanza kumubembeleza.


Basi, Yawe alimukasirikia Solomono, kwa sababu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa Israeli, ingawa yeye alikuwa amemutokea mara mbili


Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.


Alifuata njia mbaya za mufalme Ahabu na za wafalme wengine wa Israeli kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele za Yawe,


Kwa hiyo, musiwaoeshe na wabinti zenu kwa watu hao, wala musiwaruhusu wana wenu kuwaoa wabinti zao. Pia, musishugulikie usalama au mafanikio yao, kusudi ninyi wenyewe mupate kuwa na nguvu, na mufaidie mema ya inchi hiyo na kuwaachia watoto wenu kama vile urizi milele.’


Ee Yawe, ninawachukia wanaokuchukia; ninawazarau sana wale wanaokuasi!


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


Mufanye angalisho musifanye agano na wakaaji wa inchi munayoiendea, maana hiyo itakuwa mutego kati yenu.


Vijana wenu wakioa wabinti zao, na hao wabinti wanaoabudu miungu yao, watawashawishi vijana wenu kufuata miungu yao.


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”


Lakini niko na neno moja juu yako: wewe hauna tena upendo kwangu kama vile mbele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ