Makundi ya ngamia yataifunika inchi yako, wana wa ngamia kutoka Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Seba. Watakuletea zahabu na ubani, wakitangaza sifa za Yawe.
Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.
Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kutokana na uzuri wako, maana uzuri wako ulikamilika kwa sababu ya utukufu niliokujalia. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Wakaaji wa Seba na Dedani pamoja na wachuuzi wa Tarsisi na wa vijiji vyake watakuuliza: Umekuja kunyanganya? Umekusanya kundi lako la waaskari kwa kushambulia na kutwaa mateka na kubeba feza na zahabu, makundi ya nyama na vitu, na kuondoka na vitu vingi?
Vilevile kwa Siku ya hukumu malkia toka kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikia maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kumupita Solomono!
Vilevile kwa Siku ya hukumu, Malkia toka Kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikiliza maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Solomono!