Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Malkia wa Seba aliposikia sifa za Solomono, kwa sababu ya jina la Yawe, alimwendea Solomono kwa kumujaribu kwa maulizo magumu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 10:1
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Wana wa Rama walikuwa Seba na Dedani.


Yokisani alizaa Seba na Dedani. Wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletusi na Waleumi.


Watu wa inchi zote walikuwa na hamu ya kumwendea Solomono kwa kusikiliza hekima yake ambayo Mungu alikuwa amemujalia.


Watu kutoka mataifa yote, na wafalme wote waliopata kusikia habari juu ya hekima yake, walikuja kumusikiliza.


Kisha Mungu akamwambia mwanadamu: Sikia! Kumwogopa Bwana ndiyo hekima, na kujitenga na uovu ndiyo maarifa.


Wasafiri toka Tema wanatafutatafuta, wasafiri toka Sheba wanatumainia.


Maneno yangu ni mazitomazito; mawazo yangu ni ya hekima.


Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.


Mufalme aishi maisha marefu; apokee zawadi ya zahabu kutoka Sheba; watu wamwombee kwa Mungu siku zote, na kumutakia baraka muchana kutwa.


Makundi ya ngamia yataifunika inchi yako, wana wa ngamia kutoka Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Seba. Watakuletea zahabu na ubani, wakitangaza sifa za Yawe.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kutokana na uzuri wako, maana uzuri wako ulikamilika kwa sababu ya utukufu niliokujalia. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Wakaaji wa Seba na Dedani pamoja na wachuuzi wa Tarsisi na wa vijiji vyake watakuuliza: Umekuja kunyanganya? Umekusanya kundi lako la waaskari kwa kushambulia na kutwaa mateka na kubeba feza na zahabu, makundi ya nyama na vitu, na kuondoka na vitu vingi?


Vilevile kwa Siku ya hukumu malkia toka kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikia maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kumupita Solomono!


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.


Ilitokea vile kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii: “Nitasema nao kwa mifano, nitawaambia maneno yaliyofichwa tangu kuumbwa kwa dunia.”


Hakusema nao pasipo kutumia mifano lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao, aliwafasiria mambo yote.


Vilevile kwa Siku ya hukumu, Malkia toka Kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikiliza maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Solomono!


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ