Wakati Abusaloma alipokuwa akitoa sadaka, alituma ujumbe katika muji wa Gilo kwa kumwita Ahitofeli wa muji wa Gilo, aliyekuwa mushauri wa mufalme Daudi. Uasi wa Abusaloma ukazidi kupata nguvu na watu waliojiunga naye wakazidi kuongezeka.
Makuhani Zadoki na Abiatari wako pamoja nawe katika muji. Basi, chochote utakachosikia kutoka katika nyumba ya mufalme, uwaambie makuhani Zadoki na Abiatari.
Mufalme Solomono akamwuliza mama yake: “Kwa nini unataka nimupe Abisagi? Hii ni sawa kabisa na kumutakia ufalme wangu! Kumbuka kwamba yeye ni mukubwa yangu, na si ile tu, kuhani Abiatari na jemadari Yoabu mwana wa Zeruya, wako upande wake!”
Halafu Daudi akasema: “Mutu atakayetangulia kuwapiga Wayebusi, atakuwa mukubwa na jemadari katika jeshi.” Basi Yoabu mwana wa Zeruya, akakuwa wa kwanza kuwashambulia, hivyo akakuwa mukubwa.