Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 1:53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

53 Basi, mufalme Solomono akaagiza Adonia aitwe kutoka katika hema, akuje kwake. Adonia akafika mbele ya mufalme, akainama kwa heshima. Mufalme akamwambia: “Kwenda kwa nyumba yako.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 1:53
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


Lakini mufalme akasema: “Abusaloma aishi kwake. Asikuje hapa kuniona.” Kwa hiyo, Abusaloma akakuwa anaishi mbali, kwake na hakumwona mufalme Daudi.


Basi, Abusaloma aliishi Yerusalema kwa muda wa miaka miwili mizima bila kumwona mufalme Daudi.


Kwa hiyo Yoabu akaenda na kumwelezea mufalme maneno hayo yote, naye akamwita Abusaloma. Abusaloma akaingia kwa mufalme, akaanguka uso mpaka chini mbele ya mufalme. Na mufalme akamubusu Abusaloma.


Batiseba aliinama kwa heshima mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: “Unataka nini?”


Batiseba akainama uso mpaka chini, kwa heshima mbele ya mufalme, na kusema: “Bwana wangu mufalme Daudi aishi milele!”


Mufalme Solomono akasema: “Nikimwona kuwa mwaminifu basi, hatapata hasara yoyote. Lakini nikimwona kuwa mwovu, hakika atakufa.”


Daudi alipokaribia kufa, alimwita mwana wake Solomono, akamupa maagizo akisema:


Halafu mufalme akaagiza Simei aitwe, akamwambia: “Ujijengee nyumba humu Yerusalema, ukae hapa bila kwenda pahali pengine popote.


Mwana wangu, uwaheshimu Yawe na mufalme, wala usishirikiane na waasi,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ