Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 1:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Mufalme Solomono akasema: “Nikimwona kuwa mwaminifu basi, hatapata hasara yoyote. Lakini nikimwona kuwa mwovu, hakika atakufa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 1:52
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mwanamuke akamwambia: “Tafazali, mufalme, uniombee kwa Yawe, Mungu wako, kusudi yule ndugu yangu ambaye angelipiza kisasi kutokana na mauaji ya mwana wangu hatafanya kosa lingine kubwa la kumwua yule mutoto wangu mwingine.” Mufalme Daudi akamwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, hakuna hata unywele mumoja wa mwana wako utakaoanguka chini.”


Mufalme Solomono akapata habari kwamba Adonia alikuwa amekimbilia ndani ya hema, na kwamba anashikilia pembe za mazabahu akisema: “Sitaondoka hapa mpaka mufalme Solomono atakaponihakikishia kwamba hataamuru niuawe.”


Basi, mufalme Solomono akaagiza Adonia aitwe kutoka katika hema, akuje kwake. Adonia akafika mbele ya mufalme, akainama kwa heshima. Mufalme akamwambia: “Kwenda kwa nyumba yako.”


Mwovu hana tumaini la kutoka katika giza; mwisho wake ni kufa kwa upanga.


Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.


Mwenye haki anajua yanayokuwa katika nyumba ya waovu: waovu wanaangushwa chini na kuangamia.


Na kwa upande wenu, yeye anajua hesabu ya nywele zote za vichwa vyenu.


Lakini hata unywele mumoja wa kichwa chenu hautapotea.


Basi ninawasihi ninyi mukule chakula, kwa sababu kitawafalia kusudi musikufe. Kwa maana hakuna mumoja kati yenu atakayepatwa na hasara yoyote hata kidogo.”


Lakini watu wakamwambia Saulo: “Kwa nini Yonatani, aliyeletea Waisraeli ushindi huu mukubwa, auawe? Haiwezikani hata kidogo. Kama vile Yawe anavyoishi, hata unywele mumoja wa kichwa chake hautaanguka chini. Alichokifanya leo, amekifanya kwa musaada wa Yawe.” Kwa hiyo, watu walimukomboa Yonatani naye hakuuawa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ