Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 1:5
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Adonia muzaliwa wa ine, mama yake alikuwa Hagiti; Sefatia muzaliwa wake wa tano, mama yake alikuwa Abitali;


Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?


Binti yule, alikuwa muzuri sana. Basi, akaanza kumutumikia na kumutunza mufalme, lakini mufalme hakumujua kimwili.


Nyuma, Adonia mwana wa Hagiti, alimwendea Batiseba, mama ya Solomono. Batiseba akamwuliza: “Unaleta habari ya amani?” Adonia akamujibu: “Ndiyo, ninaleta habari ya amani.


Adonia akamwambia: “Unajua kwamba ni mimi ndiye ningalikuwa mufalme, na hata Israeli yote ilikuwa inanitazamia nikuwe mufalme. Lakini, mambo yakageuka na ndugu yangu akanipindua, kwa sababu hayo ndiyo yaliyokuwa mapenzi ya Yawe.


Sasa basi, kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyeniweka na kuniimarisha katika ufalme wa baba yangu Daudi na kutimiza ahadi yake ya kunipa kiti cha kifalme mimi na wazao wangu, Adonia atakufa leo!”


Yawe amenijalia wana wengi, na kati ya hao wote, amemuchagua Solomono mwana wangu, aikae juu ya kiti cha kifalme cha ufalme wa Yawe atawale.


Mufalme Daudi akawaambia wale watu wote waliokusanyika: “Solomono mwana wangu, ambaye peke yake amechaguliwa na Mungu, angali bado mudogo, hana maarifa mengi na kazi hii ni kubwa. Nyumba atakayojenga si ya mwanadamu, lakini ni ya Mungu, Yawe.


Lakini ungali unaonyesha kiburi juu ya watu wangu, wala hauwaachi waondoke.


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Inchi yao imejaa feza na zahabu, akiba yao ni kubwa zaidi. Inchi yao imejaa farasi, magari yao ya vita hayana hesabu.


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


“Museme hapa hapa mbele ya wanainchi wote wa Sekemu: Jambo gani ni jema kwenu, kwamba watoto wote makumi saba wa kiume wa Yerubali wawatawale au mutoto mumoja? Mukumbuke kwamba mimi ni damu yenu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ