Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”
Umwendee mufalme Daudi, umwulize: ‘Bwana wangu mufalme, si uliniapia mimi mujakazi wako ukisema: Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme? Imekuwa namna gani basi, sasa Adonia anatawala?’
Yoramu alipoikalia kiti cha kifalme na utawala wake ulipokuwa umekwisha kuimarika, yeye akawaua wandugu zake wote kwa upanga, na vilevile wakubwa wamoja wa Israeli.
Lakini wakati walimaji walipomwona yule mwana, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’
Akafuatana nao kwenda Ofura kwa baba yake naye akawaua wandugu zake wote makumi saba juu ya jiwe moja. Lakini Yotamu, mwana mudogo wa Yerubali aliponyoka kufa, maana alijificha.