Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.
Lakini ukatae kuandika wajane wanaokuwa wangali vijana katika hesabu ile kwa maana wanapovutwa na tamaa ya kutaka kuolewa, wanaacha kumutumikia Kristo.
Lakini kama mwamini yeyote akiwa na wajane katika jamaa lake, anapaswa kuwasaidia kusudi kanisa lisilemewe. Na hivi kanisa nalo litaweza kuwasaidia wale wajane wasiokuwa na tegemeo lolote.