Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.
Vilevile ni sherti kujua kwamba Sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, lakini kwa ajili ya watenda mabaya, waasi, watu wasiomuheshimu Mungu, wenye zambi, nao wenye kuchafua vitu vitakatifu na kukufuru, na kwa ajili ya wale wanaowaua wababa zao au wamama zao, na wauaji wowote.
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.
Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.
Timoteo, uchunge vizuri kile ulichopewa kwa kulinda, ukiepuka maneno ya kidunia na mabishano yasiyokuwa na maana juu ya ile watu wengine wanayoita kuwa ni elimu lakini ni uongo.
na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.
Neema hii inatufundisha kwamba tuache uovu na tamaa za dunia, na kuishi katika dunia hii ya sasa katika ukadirifu, katika haki na kushikamana na ibada.
Lakini uepuke mabishano ya upumbafu, hadisi za vizazi vya babu, na magomvi pamoja na mapingano juu ya Sheria, kwa sababu mambo hayo hayana mafaa, nayo ni ya bure.