musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”
Lakini kwa ngambo ya watu wa mataifa mengine walioamini, tumekwisha kuwaandikia juu ya mambo tuliyoamua. Tumewaamuru kwamba wasikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; wasikule damu wala nyamafu; na waepuke uasherati.”
Kufuatana na vile ninaungana na Bwana Yesu, ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachohesabiwa kichafu katika hali yake ya asili. Lakini kama mutu akihesabu kwamba kitu fulani ni kichafu, basi kitu kile ni kichafu kwake.
Usiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya maneno ya chakula. Hakika vyakula vyote vinaruhusiwa kukuliwa, lakini ni vibaya kwa mutu kula chakula kinachoweza kukwaza mwingine.
Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.
Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.
Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.