Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.
Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.