Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Timoteo 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ukae kule Efeso sawa vile nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia. Na kule uwazuize wale watu wanaofundisha mafundisho ya uongo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Timoteo 1:3
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipofika Efeso, Paulo akawaacha wale wenzake kule. Naye mwenyewe akaingia ndani ya nyumba ya kuabudia na kubishana na Wayuda.


Alipoagana nao, akawaambia: “Kama Mungu akitaka nitarudi huku kwenu tena.” Halafu akaondoka Efeso, akisafiri kwa njia ya chombo.


Kwa maana imependeza makanisa ya Makedonia na ya Akaya kukusanya mali kwa kuwasaidia wamasikini wanaokuwa kati ya watu wa Mungu kule Yerusalema.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Hii inatokana na kuona jinsi munavyomukubali mutu yeyote anayekuja kwenu na kuwahubiri habari za Yesu mwingine asiyekuwa yule sisi tuliyemuhubiri. Na zaidi ya hii munakubali upesi kupokea roho ingine na ujumbe mwingine vinavyokuwa tofauti na Roho au Habari Njema muliyopokea toka kwetu.


Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


Nami ninamutumainia Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kuwaona bado kidogo.


Hayo ndiyo maneno unayopaswa kuagiza na kufundisha.


Kama ukiwaelezea waziwazi wandugu maneno hayo, utakuwa mutumishi mwema wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa kiroho na maneno ya imani na mafundisho mazuri uliyoshika kabisa.


Hayo ndiyo maneno unayopaswa kuwaagiza wajane kusudi wasikuwe na mashitaki.


Kwa maana kupenda feza ni shina la mabaya yote. Kwa ajili ya kuzitamani watu wamoja wanaanguka katika imani yao, na wanajiumiza mioyo wakijiletea huzuni nyingi.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Kama mutu akifundisha mafundisho mengine, naye hakubali maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo wala mafundisho yanayolingana na dini yetu,


Bwana amusikilie huruma kwa Siku ile! Unajua vizuri sana vilevile mambo yote aliyonitendea kule Efeso.


Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ