Mutu mumoja akatoka Bali-Salisa, akamuletea Elisha mikate makumi mbili iliyotengenezwa kwa shayiri ya malimbuko ya mavuno ya mwaka ule na masuke mabichi ya ngano katika gunia. Elisha akamwagiza Gehazi awape watu wakule.
Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”
Mufalme wa Aramu akamwambia: “Twaa barua hii umupelekee mufalme wa Israeli.” Hivyo Namani akaondoka, akipeleka vikoroti elfu makumi tatu vya feza, vikoroti elfu sita vya zahabu na nguo kumi za sikukuu.
Hazaeli akapakia zawadi za kila aina ya mazao ya Damasiki kipimo cha mizigo ya ngamia makumi ine na kumupelekea Elisha. Alipofika kwa Elisha alimwambia: “Mutumishi wako, Beni-Hadadi, mufalme wa Aramu amenituma kwako. Yeye anauliza: ‘Nitapona ugonjwa huu?’ ”
Mumenizaraulisha mbele ya watu wangu kusudi mupate vitanga vya shayiri na chakula kidogo. Munawaua watu wasiostahili kufa na kuwaacha wazima wanaostahili kuuawa, kwa uongo wenu munaowaambia watu wangu, nao wanawaaminia.