Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 9:6
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Leo nilipofika kwenye kisima nikaomba: ‘Ee Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ninakuomba unisaidie leo katika safari yangu na umutendee Abrahamu bwana wangu mema.


Mufalme Daudi akamwambia tena Zadoki: “Twaa mwana wako Ahimasi na Yonatani mwana wa Abiatari, murudi katika muji kwa amani.


Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Elisha, nabii wa Mungu, alipopata habari kwamba mufalme wa Israeli amepasua nguo zake, alituma ujumbe kwa mufalme, akamwuliza: “Kwa sababu gani umepasua nguo zako? Umutume mutu huyo kwangu, kusudi apate kujua kwamba kuna nabii katika Israeli!”


Elisha akauliza: “Liliangukia wapi?” Mutu huyo akamwonyesha. Elisha akakata kijiti na kukitupa ndani ya maji na palepale shoka likaelea juu ya maji.


Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:


Ninyi ni washuhuda wetu, na Mungu vilevile anashuhudia kwamba tulipokaa kati yenu ninyi waamini, tuliishi katika utakatifu na haki, na bila kosa.


Muwape heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Mukuwe na amani kati yenu.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Siku moja, mutu wa Yawe alimwendea Eli, akamwambia: “Yawe amesema hivi: Nilijijulisha kwa jamaa ya Haruni, babu yako, walipokuwa watumwa wa mufalme wa Misri katika inchi ya Misri.


Yule mutumishi akamujibu Saulo: “Ona, mimi nina vikoroti vine vya shekeli. Nitamupa huyo mutu wa Mungu kusudi atuambie juu ya safari yetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ