Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wakawatafuta kwenye inchi ya milima ya Efuraimu na eneo la Shalisa, lakini hawakuwaona kule. Halafu wakafika Salimu, na kule hawakuwaona. Wakawatafuta katika inchi ya Benjamina, hata hivyo hawakuwapata.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 9:4
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutoka Padani-Aramu, Yakobo akafika salama kwa muji wa Sekemu, katika inchi ya Kanana, akapiga kambi yake karibu na muji ule.


Mutu mumoja akatoka Bali-Salisa, akamuletea Elisha mikate makumi mbili iliyotengenezwa kwa shayiri ya malimbuko ya mavuno ya mwaka ule na masuke mabichi ya ngano katika gunia. Elisha akamwagiza Gehazi awape watu wakule.


Yoane vilevile alikuwa akibatiza kule Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu kule kulikuwa maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.


Naye Eleazari mwana wa Haruni, akakufa na kuzikwa Gibea, muji ambao mwana wake Finehasi alikuwa amepewa katika inchi ya milima ya Efuraimu.


Kulikuwa mutu mumoja kule katika milima ya Efuraimu, jina lake Mika.


Wakati ule hakukukuwa bado mufalme katika Israeli. Kulikuwa Mulawi mumoja aliyeishi kama mugeni mbali katika eneo la milima ya Efuraimu. Mutu yule alitwaa habara kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda.


Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.


Siku moja, punda wa Kisi, baba ya Saulo, walipotea. Hivyo, Kisi akamwambia Saulo: “Ukamate mutumishi mumoja, uende kuwatafuta punda.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ