Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 9:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Kesho yake asubui mapema, Samweli alimwita Saulo kutoka juu ya dari: “Amuka, kusudi nikusindikize urudi kwa nyumba.” Saulo aliamuka, na wote wawili, yeye na Samweli, wakatoka na kwenda katika barabara.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 9:26
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.


Walipokuwa wamesafiri mwendo mufupi tu kutoka muji, Yosefu akamwambia musimamizi wa nyumba yake: “Haraka! Ufuate wale watu, na utakapowakuta, uwaulize: ‘Kwa nini mumelipa mema muliyotendewa kwa maovu? Kwa nini mumeiba kikombe cha bwana wangu ambacho


Basi, simama uwatakase watu, uwaambie wajitakase na kujitayarisha kwa siku ya kesho, maana mimi Yawe, Mungu wa Israeli, ninasema hivi: ‘Kati yenu kuna vitu vilivyotolewa viangamizwe. Hamuwezi kuwashinda waadui zenu mpaka vitu hivyo vimeondolewa kati yenu!


Akamwambia: “Simama tuende.” Lakini yeye hakujibu kitu. Akamukamata, akamuweka juu ya punda wake na kumupeleka mpaka kwake.


Waliporudi katika muji kutoka kwenye nafasi ya ibada juu ya mulima, alizungumuza na Saulo juu ya dari. Na Saulo akalala kule.


Walipofika mwisho wa muji, Samweli akamwambia Saulo: “Umwambie yule kijana atangulie mbele yetu.” Kijana alipokwisha ondoka, Samweli akaendelea kusema: “Ngoja kidogo, nami nitakufunulia yale Mungu aliyosema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ