Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.
Basi, watu wakaenda kuleta matawi, wakajenga vibanda kila mutu kwenye dari na kwenye baraza ya nyumba yake, kwenye baraza za nyumba ya Mungu, kwenye uwanja wa kiwanja cha Mulango wa Maji na kiwanja cha Mulango wa Efuraimu.
Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.
Lakini kwa kuona walikosa njia ya kumwingiza ndani, kwa sababu ya wingi wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondosha matebura na kumushusha yule mugonjwa katikati ya watu, akiwa juu ya kipoyi chake, hata wakamufikisha mbele ya Yesu.
Kesho yake asubui mapema, Samweli alimwita Saulo kutoka juu ya dari: “Amuka, kusudi nikusindikize urudi kwa nyumba.” Saulo aliamuka, na wote wawili, yeye na Samweli, wakatoka na kwenda katika barabara.