18 Hapo Saulo alimwendea Samweli aliyekuwa karibu na mulango wa muji na kumwuliza: “Ninakuomba unionyeshe nyumba ya mwonaji.”
Samweli alipomwona tu Saulo, Yawe alimwambia: “Huyu ndiye mutu yule niliyekuambia. Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
Samweli akamujibu: “Mimi ndiye mwonaji. Munitangulie kwenda kwenye nafasi ya kuabudia maana leo mutakula pamoja nami. Kesho asubui maulizo yote unayokuwa nayo nitayajibu.