Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 “Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 9:16
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Maombi ya mutu anayekuwa katika taabu ambaye anamutolea Yawe malalamiko yake.


Hata hivyo Mungu aliona taabu yao, wakati aliposikia kilio chao;


Uangalie mateso yangu na taabu yangu; unisamehe zambi zangu zote.


Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.


Kisha binamu yangu Hanameli akanifikia katika baraza la walinzi kama alivyonifahamisha Yawe, akaniambia: Nunua shamba langu linalokuwa kule Anatoti katika inchi ya Benjamina maana wewe uko na haki ya kulikomboa. Ulinunue kwa faida yako. Basi nikajua kwamba neno hili ni la Yawe.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Hivyo, Saulo na watu wake wakajipanga na kuingia katika vita na Wafilistini. Lakini Wafilistini walianza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kwa muvurugiko mukubwa.


Hivyo Yawe aliwapa Waisraeli ushindi. Vita ilienea mpaka kupita Beti-Aweni.


Samweli alimwambia Saulo: “Yawe alinituma kukupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme wa watu wake Waisraeli. Sasa sikiliza maneno ya Yawe.


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Umwalike Yese kwenye sadaka hiyo nami nitakuonyesha la kufanya. Utamupakaa mafuta kwa ajili yangu mutu yule nitakayekutajia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ