Maana wewe, ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, umenifunulia mimi mutumishi wako, ukisema: ‘Nitakujengea nyumba’; ndiyo maana nina uhodari wa kutoa ombi hili mbele yako.
Yonatani akamujibu: “Jambo hilo lipite mbali nawe. Hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo lolote, likuwe kubwa au dogo, bila kunielezea. Hata jambo hili hawezi kunificha. Sivyo inavyokuwa hata kidogo.”
Hivyo Saulo na mutumishi wake walikwenda katika muji. Walipokuwa wanaingia katika muji, walimwona Samweli akitoka katika muji, na anaelekea kwenda kwenye nafasi ya kuabudia.