10 Saulo akamujibu: “Hilo ni jambo zuri; basi, tuende.” Hivyo, wakaenda kwenye muji mutu yule wa Mungu alimokuwa anakaa.
Baba mudogo wa Saulo alipowaona Saulo na mutumishi, akawauliza: “Mulikuwa wapi?” Saulo akajibu: “Tulikwenda kuwatafuta punda, na tulipoona hawapatikani, tulikwenda kumwona Samweli.”
Walipokuwa wanapanda mulima kuelekea katika muji, wakakutana na wabinti waliokuwa wakienda kuteka maji. Wakawauliza wabinti wale: “Mwonaji yuko katika muji?”
(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).