Nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa, nawe haumwonyi au kumwambia aache mwenendo wake mubaya apate kuyaokoa maisha yake, basi, mutu huyo mwovu atakufa kwa uovu wake; lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.
Mufalme hapaswi kunyanganya hata kidogo mali ya watu. Sehemu ya inchi yoyote anayowapa watoto wake wa kiume inapaswa kutokana na eneo lake mwenyewe. Hivyo hatawatesa watu wangu kwa kuwanyanganya urizi wao.
Kisha, Samweli aliwaelezea watu juu ya mapaswa na haki za mufalme, akaziandika katika kitabu ambacho alikiweka mbele ya Yawe. Kisha, Samweli aliwaaga watu wote, kila mutu aende kwake.
Kulikuwa vita kali na Wafilistini kwa muda wote Saulo alipokuwa mufalme. Na kila mara Saulo alipomupata mutu mwenye nguvu au shujaa alimukamata apate kujiunga na waaskari wake.
wala juu ya vitu ambavyo watu walipaswa kuwapa makuhani. Kila mara mutu alipokuwa anatolea sadaka yake, mutumishi wa kuhani alikuja na kanya yenye meno matatu; na wakati nyama ikiwa bado inatokota,
Tangu nilipowatoa Misri, wameniacha mimi, wamekuwa wakiitumikia miungu mingine mpaka leo. Sasa hayo matendo ambayo wamekuwa wakinitendea mimi, ndiyo wanayokutendea na wewe.