Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yawe akamwambia: “Sikiliza kila kitu ambacho watu wanakuambia; maana hawajakukataa wewe, lakini wamenikataa mimi kuwa mufalme juu yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 8:7
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Basi, nitawaletea taabu; zile hasara zote wanazoogopa zitawapata; maana nilipoita hakuna aliyeitika, niliposema hawakunisikiliza. Lakini walifanya maovu mbele yangu, walichagua yale ambayo hayanipendezi.


Kila mwaka wa saba, kila mumoja wenu atamwachilia huru ndugu yake Muyuda aliyeuzishwa kuwa mutumwa kwa muda wa miaka sita. Munapaswa kuwaachilia huru, wasiwatumikie tena. Lakini babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio.


akiniambia hivi: Wewe mwanadamu ninakutuma kwa Waisraeli, taifa la waasi ambao wameniasi. Wameendelea kunikosea mimi mpaka leo sawa vile babu zao walivyofanya.


Lakini Waisraeli watakataa kukusikiliza, maana hawataki kunisikiliza mimi. Watu wote wa Israeli ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu.


Basi, Mungu akamufikia Balamu usiku ule, akamwambia: Kama watu hawa wamekuja kukuita, kwenda pamoja nao, lakini fanya tu kile nitakachokuambia.


“Mutu anayewapokea ninyi, ananipokea mimi; naye anayenipokea, anamupokea yule aliyenituma.


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


Lakini wanainchi wenzake walimuchukia. Kwa hiyo wakatuma wajumbe kumufuata nyuma waende kusema: ‘Hatutaki mutu huyu kuwa mufalme wetu.’


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


Kweli, kweli ninawaambia: mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake, wala mujumbe si mukubwa kuliko yule aliyemutuma.


Gideoni akawajibu: “Mimi sitakuwa mutawala wenu wala mwana wangu hatakuwa mutawala wenu. Yawe ndiye atakayekuwa mutawala wenu.”


Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”


Samweli akawaambia Waisraeli wote: “Maneno yote muliyoniambia, nimeyasikiliza. Nimemusimika mufalme juu yenu.


Lakini mulipomwona mufalme Nahasi wa Waamoni amekuja kuwashambulia, mukamukataa Yawe ambaye ndiye Mufalme wenu, mukaniambia: ‘Hapana! Mufalme ndiye atakayetutawala’.


Yawe akamwambia Samweli: “Uwasikilize na uwapatie mufalme.” Kisha Samweli akawaambia Waisraeli warudie kwao, kila mutu katika muji wake.


Tangu nilipowatoa Misri, wameniacha mimi, wamekuwa wakiitumikia miungu mingine mpaka leo. Sasa hayo matendo ambayo wamekuwa wakinitendea mimi, ndiyo wanayokutendea na wewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ