Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Samweli aliwaambia: “Hivi ndivyo mufalme wenu atakayewatawala atakavyowatendea: wana wenu atawafanya wakuwe waendeshaji wa magari yake, na wengine kuwa waaskari wapanda-farasi wake, na wengine watapiga mbio mbele ya magari yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 8:11
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi. Alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili ambao aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita, na kule Yerusalema.


Hao vijana wakamujibu: “Watu hao waliokuambia baba yako aliwabebesha muzigo muzito, wakakuomba uwapunguzie muzigo ule, wewe uwaambie hivi: ‘Kidole changu kidogo cha mwisho ni kinene zaidi kuliko kiuno cha baba yangu.


“Baba yako alitubebesha muzigo muzito. Basi, utupunguzie muzigo huo muzito wa baba yako, nasi tutakutumikia.”


Pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu alitengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa wachungaji wa mulango wa nyumba ya kifalme.


Nguvu ya Yawe ikamufikia Elia, naye akajitayarisha kusafiri, akakimbia na kumutangulia Ahabu kuingia ndani ya muji Yezereheli.


Kisha, Samweli aliwaelezea watu juu ya mapaswa na haki za mufalme, akaziandika katika kitabu ambacho alikiweka mbele ya Yawe. Kisha, Samweli aliwaaga watu wote, kila mutu aende kwake.


Kulikuwa vita kali na Wafilistini kwa muda wote Saulo alipokuwa mufalme. Na kila mara Saulo alipomupata mutu mwenye nguvu au shujaa alimukamata apate kujiunga na waaskari wake.


Naye Saulo akawaambia watumishi wake: “Sasa ninyi watu wa kabila la Benjamina munisikilize, munazani kwamba huyu Daudi mwana wa Yese atamupa kila mumoja wenu mashamba ya mizabibu na mashamba mengine? Au munazani kwamba atamufanya kila mumoja wenu kuwa mukubwa wa waaskari maelfu au mukubwa wa waaskari mamia?


Basi, uwasikilize, lakini uwaonye vikali, na uwaelezee waziwazi jinsi mufalme atakayewatawala atakavyowatendea.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ