Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Samweli alipokuwa anatolea ile sadaka ya kuteketezwa, Wafilistini walikaribia kuwashambulia Waisraeli. Lakini Yawe akatoa sauti kubwa ya ngurumo juu ya Wafilistini, na kuwavuruga Wafilistini, nao wakashindwa mbele ya Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 7:10
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliwapiga waadui mishale yake, akawatawanya; alirusha umeme mukali, akawakimbiza.


Sauti ya Yawe inasikilika juu ya maji; Mungu mutukufu anapiga radi, sauti ya Yawe inasikilika juu ya bahari!


Sauti ya Yawe ni yenye nguvu, sauti ya Yawe ni yenye mamlaka.


Akawashinda waadui zake; akawafezehesha kwa milele.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Waadui zenu wakiwashambulia, Yawe atawapa ushindi juu yao. Wakikuja kuwashambulia kwa njia moja watawakimbia kwa njia saba.


Naye Yawe akawatia hofu kubwa mbele ya Waisraeli ambao waliwaua watu wengi kule Gibeoni wakiwakimbia kwenye njia ya muteremuko wa Beti-Horoni mpaka Azeka na Makeda ambako vilevile waliwaua watu wengi sana.


Baraka akafanya mashambulizi, naye Yawe akamukimbiza Sisera na waaskari wake wote mbele ya Baraka kwa upanga. Sisera akatoka katika gari lake, akakimbia kwa miguu.


Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita, zilifuata njia zao zikapigana na Sisera.


Walijichagulia miungu mipya, kukakuwa vita katika inchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu elfu makumi ine wa Israeli.


Sasa si wakati wa kuvuna ngano? Lakini mimi nitamwomba Yawe alete radi na mvua, nanyi mutatambua na kuona kwamba uovu wenu muliotenda mbele ya Yawe kwa kujitakia mufalme, ni mukubwa.”


Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.


Waadui za Yawe watavunjwa vipandevipande; atanguruma juu yao kama radi mbinguni. Yawe ataihukumu dunia yote, atamupa nguvu mufalme wake, na atautukuza uwezo wa muchaguliwa wake.


Waisraeli walitoka Misipa na kuwafuatilia Wafilistini mpaka karibu na muji wa Beti-kari, wakawaangamiza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ