Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini muangalie. Ikiwa gari hilo linakwenda moja kwa moja kuelekea inchi yake, ni kusema kwenye muji wa Beti-Semesi, basi, pale tutajua kwamba aliyetuletea pigo hili ni Mungu wa Israeli. Lakini kama haliendi kule, basi, tutajua kwamba sio mukono wake uliotupiga, lakini hasara hii imetupata kwa bahati mbaya.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 6:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule kijana akamujibu: “Kwa bahati, nilikuwa juu ya mulima Gilboa. Nilimwona Saulo akiegemea mukuki wake na magari ya waaskari wapanda-farasi ya waadui zake yalikuwa yanamusonga sana.


Kwa hiyo, Yoasi, mufalme wa Israeli akatoka akapambana uso kwa uso na Amazia, mufalme wa Yuda katika vita kule Beti-Semesi, katika inchi ya Yuda.


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Kukatokea kuhani mumoja akishuka katika njia ile ile. Wakati alipomwona yule mutu, akapita pembeni na kujiendea.


ambako ulipinda upande wa magaribi kuelekea Seiri; ukapita kaskazini ya mulima wa Yerimu, ni kusema Kesaloni, na kuteremuka mpaka Beti-Semesi ambapo ulipita karibu na Timuna.


Aini pamoja na mbuga zake za malisho, Yuta pamoja na mbuga zake za malisho na Beti-Semesi pamoja na mbuga zake za malisho. Jumla ya miji hiyo inayokuwa katika maeneo ya makabila hayo mawili ni tisa.


Walifanya kama walivyoambiwa; walitwaa ngombe wawili wenye kunyonyesha na kuwafunga kwenye gari, na vitoto vyao wakavifunga katika zizi.


Wale ngombe walikwenda moja kwa moja kuelekea muji wa Beti-Semesi bila kupinda kushoto au kuume, walikuwa wanalia walipokuwa wanakwenda. Wale wafalme watano wa Wafilistini waliwafuata mpaka kwenye mupaka wa Beti-Semesi.


Wao wakawaambia: “Mukirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, musilirudishe mikono mitupu. Lakini munapolirudisha mupeleke na sadaka ya malipo ya kosa kwa kuondoa makosa yenu. Mukifanya hivyo mutapona, nanyi mutafahamu kwa nini amekuwa akiwaazibu kwa mufululizo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ