Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi mufanye sanamu zenu za majipu na sanamu za panya, vitu ambavyo vinaangamiza inchi yenu, nanyi mutamutukuza Mungu wa Israeli. Labda ataacha kuwaazibu ninyi wenyewe, miungu yenu na inchi yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 6:5
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mumupe Yawe heshima, enyi jamii zote za watu, mutangaze utukufu na nguvu yake.


Mumupe Yawe heshima ya utukufu wa jina lake; mulete sadaka na kuingia katika nyumba yake. Mumwabudu Yawe katika Pahali Patakatifu pake.


Wewe uliniokoa kutoka mashambulizi ya watu, ukanifanya kuwa mutawala wa mataifa. Watu nisiowajua walinitumikia.


Muchana na usiku mukono wako ulinilemea; nguvu zangu zikakwisha, kama maji yanavyokauka wakati wa kipwa.


Niko kama bubu, sisemi kitu, kwa maana wewe ndiwe uliyetenda hayo.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya mainzi, wewe, wakubwa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya mainzi na inchi yote ya Misri vilevile.


Basi, mufalme wa Misri akasema: “Nitawaacha mujiendee kutoa sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, katika jangwa. Lakini musiende mbali sana. Muniombee mimi.”


Musa akamujibu mufalme wa Misri: “Basi! Unaweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee wakubwa wako na watu wako. Nitamwomba awaangamize vyura hawa wanaokuwa katika nyumba zenu. Watabaki tu katika muto Nili!”


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Wote wanaokaa katika inchi za mbali, wamutukuze na kumusifu Yawe.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawarudishia miaka ile iliyokuliwa na nzige, kila kitu kilichokuliwa na tunutu, parare na panzi, hilo kundi kubwa nililowaletea!


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


ambao walikuwa wanazika wazaliwa wao wa kwanza wanaume Yawe aliowaua; maana Yawe alikuwa ameiazibu hata miungu yao.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”


Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.


Halafu akasema kwa sauti kubwa: “Mumuheshimu Mungu na kumutukuza, kwa sababu saa yake ya kuwahukumu watu imetimia. Mumwabudu yule aliyeumba mbingu na dunia, bahari na chemichemi za maji.”


Watu wakaunguzwa na lile joto kali, hata wakatukana jina la Mungu anayekuwa na uwezo wa kuamuru mapigo yale. Wakakataa kugeuka toka zambi zao na kumutukuza Mungu.


Kisha wakatuma ujumbe na kukusanya wakubwa wa Wafilistini na kuwaambia: “Mulirudishe Sanduku la Mungu wa Israeli kwa nafasi yake, kusudi lisituue sisi pamoja na watu wetu.” Walifanya hivyo kwa sababu kulikuwa hofu kubwa katika muji muzima kwa sababu Mungu alikuwa anawaazibu vikali.


Lakini kisha kulipeleka kule Gati, Yawe akauazibu muji huo, akitia hofu kubwa katika muji, na akawapiga wanaume wa muji huo, vijana kama vile wazee, kwa kuwaletea majipu.


Mutwae Sanduku la Yawe na kuliweka katika gari hilo. Muweke zile sanamu za zahabu ambazo munamupelekea kama sadaka ya malipo ya makosa yenu pembeni ya Sanduku. Kisha muliache liende litakakokwenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ