Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 6:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 6:19
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Uza. Mungu akamwua palepale. Uza akakufa palepale pembeni ya Sanduku la Mungu.


Kwa hiyo, Yoasi, mufalme wa Israeli akatoka akapambana uso kwa uso na Amazia, mufalme wa Yuda katika vita kule Beti-Semesi, katika inchi ya Yuda.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Shuka chini uwaonye watu wote wasikuje kuniona. Kama sivyo wengi wao wataangamia.


Watu wakalia waliposikia habari hizi mbaya, wala hakuna aliyevaa mapambo yake.


Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Musiache ukoo wa jamaa za Kohati kati ya Walawi uangamizwe.


Lakini wazao wa Kohati hawataingia kwa kutazama vitu hivyo vitakatifu sana wakifanya hivyo watakufa.


Musikubali kuhukumiwa na mutu yeyote anayejionyesha kwa inje kuwa yeye ni munyenyekevu na mwenye kuabudu malaika. Mutu wa namna hii anatia sana maana juu ya maono anayopata, naye anajitapa bure juu ya mafikiri yake ya kimutu.


Wakati wa hukumu unakaribia. Na hukumu itaanza na watu wa Mungu. Na kama hukumu inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasiotii Habari Njema ya Mungu?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ