Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 6:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Hilo gari lilielekea kwenye shamba la Yoshua, mukaaji wa Beti-Semesi. Lilipofika hapo likasimama karibu na jiwe kubwa. Watu wakalibomoa lile gari, wakatumia mbao zake kwa kuwateketeza hao ngombe ambao waliwatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 6:14
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo hiyo Gadi akamwendea Daudi, akamwambia: “Panda juu, umujengee Yawe mazabahu, katika kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.”


Naye Arauna akamwambia Daudi: “Bwana wangu mufalme, utwae chochote unachoona kinafaa na utolee sadaka. Mimi ninawatoa ngombe dume hawa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na vifaa hivi vya kupepetea na nira za ngombe kuwa kuni.


Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Basi, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi, na ule ugonjwa mukali uliowapata Waisraeli ikakoma.


Basi, Elisha akamwacha Elia, akarudilia ngombe wake, akawachinja ngombe hao na kuwapika akitumia miti ya nira kama kuni, akawapa watu, wakakula. Kisha akaondoka, akamufuata Elia na kuwa mutumishi wake.


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Kesho yake watu wakaamuka mapema, wakajenga mazabahu, wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Halafu, unijengee mimi Yawe, Mungu wako, mazabahu nzuri juu ya mwinuko ule. Kisha unitolee sadaka ya kuteketezwa ya yule ngombe dume wa pili ukitumia kuni za ile sanamu ya Ashera uliyoivunja.”


Sasa, Saulo alikuwa anatoka kwenye shamba akiwa na ngombe dume wake, akauliza: “Watu wana nini? Kwa nini wanalia?” Wakamwambia habari wajumbe waliyoleta kutoka Yabesi.


Aliniambia: ‘Uniruhusu niende kwa jamaa yangu, kwa maana wanatolea sadaka kule katika muji, na ndugu yangu amenitaka nikuwe pale. Hivyo kama nimepata kukubaliwa mbele yako, uniruhusu niende kwa wandugu zangu’. Ndiyo maana hayuko hapa kushiriki chakula cha mufalme.”


Watu wa Beti-Semesi walikuwa wanavuna ngano katika bonde. Walipoangalia juu na kuliona Sanduku la Yawe, wakafurahi sana.


Walipeleka vilevile sanamu za zahabu za panya kulingana na hesabu ya miji yote ya Wafilistini iliyotawaliwa na wakubwa watano wa Wafilistini. Miji hiyo ilikuwa yenye kuzungukwa na kuta na vijiji ambavyo havikuzungushiwa kuta. Lile jiwe kubwa kwenye shamba la Yoshua wa Beti-Semesi, pahali ambapo walilipeleka Sanduku la Yawe, ni ushuhuda wa tukio hilo mpaka leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ