ambako ulipinda upande wa magaribi kuelekea Seiri; ukapita kaskazini ya mulima wa Yerimu, ni kusema Kesaloni, na kuteremuka mpaka Beti-Semesi ambapo ulipita karibu na Timuna.
Wale ngombe walikwenda moja kwa moja kuelekea muji wa Beti-Semesi bila kupinda kushoto au kuume, walikuwa wanalia walipokuwa wanakwenda. Wale wafalme watano wa Wafilistini waliwafuata mpaka kwenye mupaka wa Beti-Semesi.
Hilo gari lilielekea kwenye shamba la Yoshua, mukaaji wa Beti-Semesi. Lilipofika hapo likasimama karibu na jiwe kubwa. Watu wakalibomoa lile gari, wakatumia mbao zake kwa kuwateketeza hao ngombe ambao waliwatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.