Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.
Nao wako na uwezo wa kufunga mbingu kusudi mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Wako vilevile na uwezo wa kugeuza maji kuwa damu, na uwezo wa kuleta mapigo ya kila namna kila wakati wanapotaka.
Sasa, enyi Wafilistini, mujipe moyo. Mukuwe hodari kusudi musipate kuwa watumwa wa Waebrania kama wao walivyokuwa watumwa wetu. Mukuwe hodari kama wanaume na kupigana.”
Wakaaji wa Asidodi walipoyaona mambo yaliyowapata, wakasema: “Mungu wa Israeli anatuazibu vikali sisi pamoja na mungu wetu Dagoni. Sanduku la Agano la Yawe haliwezi kukaa kwetu.”