Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wafilistini waliwashambulia Waisraeli, na nyuma ya mapigano makali, Waisraeli walishindwa. Waisraeli elfu ine waliuawa kwenye uwanja wa vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 4:2
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tupime na kuchunguza mwenendo wetu tupate kumurudilia Yawe.


Wataangukiana ovyo kama mutu anayekimbia vita hata kama hakuna anayewafukuza. Hamutakuwa na nguvu yoyote kwa kuwashambulia waadui zenu.


Halafu Waamaleki na Wakanana, waliokuwa wakiishi katika inchi hiyo ya milima, wakashuka, wakawashambulia na kuwashinda. Wakawafukuza mpaka muji wa Horma.


Kwa hiyo Waisraeli hawawezi kuwashinda waadui zao. Wanawakimbia waadui zao kwa sababu wamejifanya wenyewe kuwa kitu cha kuangamizwa! Sitakuwa pamoja nao tena musipoharibu vitu vinavyokuwa kati yenu vilivyotolewa viangamizwe.


Makundi ya waaskari ya Waisraeli na ya Wafilistini walijipanga tayari kupigana vita, makundi yakiwa yanaangaliana uso kwa uso.


Goliati alisimama na kuwapigia kelele waaskari wa Waisraeli, akisema: “Munafanya nini pale? Mumekuja kupigana vita? Mimi ni Mufilistini; ninyi ni watumwa wa Saulo. Muchague mutu mumoja kati yenu akuje kupigana nami.


Wakati huo, Wafilistini walikutana pamoja, wapigane na Waisraeli. Waisraeli walipiga kambi yao kule Ebeni-Ezeri, na Wafilistini wakapiga kambi yao kule Afeki.


Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.


Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ