Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 4:12
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


Basi, Tamari alijipakaa majivu kwenye kichwa, akapasua kanzu yake, akaweka mikono yake juu ya kichwa, halafu akaondoka akiwa analia kwa sauti.


Daudi alipofika kwenye kichwa cha mulima, nafasi ya kumwabudia Mungu, mutu mumoja jina lake Husai kutoka inchi ya Arki alikuja kwa kumupokea, nguo zake zikiwa zimepasuka na juu ya kichwa chake kuna mavumbi.


Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi ule wa saba, watu wa Israeli wakakusanyika, wakifunga kula na kuvaa nguo za magunia na kujipakaa udongo juu ya kichwa kwa kuonyesha majuto juu ya zambi zao.


Walipomwona kwa mbali hawakumutambua. Basi, wakaanza kulalamika na kulia. Wakapasua nguo zao, wakarusha mavumbi katika anga na juu ya vichwa vyao.


basi, nitaiharibu nyumba hii kama nilivyoharibu ile ya Shilo, na nitaufanya muji huu kuwa mufano kwa mataifa yote ya dunia yatakaoutumia kwa kutoa laana.


Siku hiyo, mutu atakayeponyoka atakuja kukupasha habari hizo.


Wataomboleza kwa uchungu wa moyo juu yako, na kulia kwa uchungu mukubwa; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kugaagaa kwenye majivu.


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ