Enyi milima ya Gilboa, musikuwe na umande au mvua juu yenu. Wala mashamba yenu yasitoe chochote siku zote. Maana kule ngao za shujaa zilichafuliwa, ngao ya Saulo haikupakaliwa mafuta.
Yosafati na waaskari wake wakaenda kukamata vitu. Wakakuta ngombe wengi, mali, nguo na vitu vingine vya bei kali. Iliwachukua muda wa siku tatu kusomba vitu hivyo, na hata hivyo, hawakuvimaliza maana vilikuwa vingi sana.
Nao Waisraeli waliokuwa upande wa pili wa bonde, na wengine waliokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, naye Saulo na wana wake wamekufa, waliihama miji yao, wakakimbia. Wafilistini wakaenda na kukaa katika miji hiyo.
Walikata kichwa cha Saulo na kumuvua silaha zake. Halafu waliwatuma wajumbe katika inchi yao yote ya Filistia kutangaza habari njema katika nyumba ya sanamu zao na kwa watu.