Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.
Daudi na watu wake pamoja na jamaa yake wakaishi na Akisi kule Gati. Daudi alikuwa na wake wawili: Ahinoamu kutoka Yezereheli na Abigaili mujane wa Nabali kutoka muji wa Karmeli.
Walikuwa wameteka wanawake na watu wote waliokuwa katika muji, wakubwa kama vile wadogo. Hao waliowateka, waliondoka nao wakiwa wazima, bila kumwua mutu yeyote.