Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake.
Sehemu wazao wa Yosefu waliyogawanyiwa kwa kura ilianzia karibu na muto Yordani, upande wa mashariki wa chemichemi ya Yeriko, na kupitia katika jangwa, hata kwenye sehemu za milima mpaka Beteli.
Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.
Basi, Yoshua akawaambia waende pahali pao pa kuvizia; nao wakajiweka upande wa magaribi wa muji wa Ai, kati ya muji wa Ai na Beteli. Lakini Yoshua akalala usiku huo katika kambi ya Waisraeli.