Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 30:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 30:14
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa kiongozi wa Wakereti na Wapeleti. Wana wa Daudi wakakuwa makuhani.


Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.


Naye mufalme amemupeleka pamoja na kuhani Zadoki, nabii Natani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, nao wamemupandisha juu ya nyumbu wa mufalme.


na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mwangalizi wa waaskari walinzi wa Daudi; wana wa Daudi walikuwa na vyeo vikubwa katika utawala wake.


basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi: Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


Halafu Yoshua akamubariki Kalebu mwana wa Yefune na kumupa muji wa Hebroni kuwa sehemu yake.


Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya inchi ya Yuda kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriati-Arba au muji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Muji huo sasa unaitwa Hebroni.


Lakini mashamba ya muji ule pamoja na vijiji vilivyouzunguka vilikuwa vimekwisha kupewa kwa Kalebu mwana wa Yefune vikuwe mali yake.


Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.


Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.


Daudi akamwuliza: “Bwana wako ni nani? Na umetoka wapi?” Yeye akamwambia: “Mimi ni kijana Mumisri. Ni mutumishi wa Mwamaleki mumoja. Bwana wangu aliniacha nyuma siku tatu zilizopita kwa maana nilikuwa mugonjwa.


Daudi akamwuliza: “Utaweza kunipeleka kwenye kundi lile?” Kijana akamujibu: “Ikiwa utaniapia kwa jina la Mungu kwamba hautaniua, wala kunitia katika mikono ya bwana wangu, nitakupeleka.”


Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ