Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.
Naye mufalme amemupeleka pamoja na kuhani Zadoki, nabii Natani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, nao wamemupandisha juu ya nyumbu wa mufalme.
basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi: Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.
Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!
Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya inchi ya Yuda kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriati-Arba au muji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Muji huo sasa unaitwa Hebroni.
Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.
Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.
Daudi akamwuliza: “Bwana wako ni nani? Na umetoka wapi?” Yeye akamwambia: “Mimi ni kijana Mumisri. Ni mutumishi wa Mwamaleki mumoja. Bwana wangu aliniacha nyuma siku tatu zilizopita kwa maana nilikuwa mugonjwa.
Daudi akamwuliza: “Utaweza kunipeleka kwenye kundi lile?” Kijana akamujibu: “Ikiwa utaniapia kwa jina la Mungu kwamba hautaniua, wala kunitia katika mikono ya bwana wangu, nitakupeleka.”
Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.