Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 30:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Vilevile walimupa kipande cha mukate wa tini na vishada viwili vya zabibu zenye kukauka. Alipomaliza kula, akapata nguvu, maana alikuwa hajakula wala kunywa kitu chochote kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 30:12
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula; wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula, kusudi wajirudishie nguvu zao. Nao muji unalia, Ee Yawe, uniangalie, ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.


na kumwambia: “Bwana, tunakumbuka kwamba wakati yule mudanganyifu alipokuwa angali muzima, alisema: ‘Kwa siku tatu kisha kufa kwangu, nitafufuka.’


Mungu akafungua pahali palipokuwa shimo kule Lehi, akatiririsha maji. Samusoni akakunywa maji hayo na nguvu zake zikamurudilia. Chemichemi hiyo ikaitwa “Kisima cha Yule Anayeita” nayo iko kule Lehi mpaka leo.


Lakini Yonatani hakusikia wakati baba yake alipowaapiza watu. Halafu akainua fimbo aliyokuwa nayo, akaichovya kwenye sega la asali, akakula asali hiyo. Hapo akajisikia kuwa na nguvu.


Wale watu waliokuwa na Daudi walimukuta mutu mumoja Mumisri katika jangwa, nao wakamupeleka kwa Daudi. Wakamupa mutu yule mukate na maji.


Daudi akamwuliza: “Bwana wako ni nani? Na umetoka wapi?” Yeye akamwambia: “Mimi ni kijana Mumisri. Ni mutumishi wa Mwamaleki mumoja. Bwana wangu aliniacha nyuma siku tatu zilizopita kwa maana nilikuwa mugonjwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ