Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Samweli naye alikuwa amelala ndani ya hekalu la Yawe karibu na Sanduku la Agano la Mungu. Taa ya Yawe ilikuwa ingali inawaka maana kulikuwa hakujapambazuka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 3:3
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.


Jambo moja nimemwomba Yawe, ninatafuta hili tu: nikae ndani ya nyumba ya Yawe siku zote za maisha yangu, niuone uzuri wa Yawe, na kutafuta maongozi yake ndani ya hekalu lake.


Sauti ya Yawe inatikisa mivule, inaongoa majani ya miti ya pori, na wote wanaokuwa katika hekalu lake wanasema: “Utukufu kwa Mungu!”


Unawaangamiza wote wanaosema uongo; unawachukia wauaji na wadanganyifu.


Utatengeneza kinara cha taa kwa zahabu safi. Tako lake na muti wa kile kinara vitakuwa kitu kimoja, vilevile na vikombe vyake. Mafundo yake na maua yake, vyote vitafuliwa kwa kipande kimoja tu cha zahabu.


Penina alikuwa akimuchokoza sana Hana kusudi amukasirikishe kwa sababu Yawe hakumujalia Hana watoto.


Siku moja, walipokuwa wamemaliza kula na kunywa katika nyumba ya Yawe kule Shilo, Hana akasimama. Wakati ule, kuhani Eli alikuwa ameikaa kwenye kiti karibu na mulango wa nyumba ya Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ