1 Samweli 3:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Watu wote katika inchi ya Israeli toka Dani, upande wa kaskazini, mpaka Beri-Seba, upande wa kusini, wakajua kwamba Samweli alikuwa nabii mwaminifu wa Yawe.
Shauri langu ni kwamba uwakusanye kwako watu wote wa Israeli tangia Dani mpaka Beri-Seba wakuwe wengi kama muchanga wa bahari, na wewe mwenyewe peke yako uende kwa vita.
Yawe alimwapia Daudi kwamba atauhamisha ufalme kutoka jamaa ya Saulo na kumupa yeye. Naye atatawala inchi ya Israeli na Yuda kutokea Dani mpaka Beri-Seba.”
Halafu Yawe alimutuma Yerubali, na kisha akamutuma Bedani, kisha Yefuta, na kwa mwisho akanituma mimi Samweli. Kila mumoja wetu aliwaokoa kutoka waadui zenu waliowazunguka, nanyi mukaishi kwa amani.