Kisha, watu wote walikwenda kumusihi Daudi akule chakula wakati ulipokuwa bado muchana. Lakini Daudi aliapa akawaambia: “Mungu aniue ikiwa nitaonja chakula au kitu chochote mpaka jua litakapotua.”
Wakati fulani mufalme Zedekia alitaka kumwona nabii Yeremia. Basi, akaagiza Yeremia aletwe kwenye mulango wa tatu wa nyumba ya Yawe. Huko, mufalme alimwambia Yeremia: Ninataka kukuuliza jambo fulani; usinifiche kitu chochote.
Basi, Balamu akarudi, akamukuta Balaki amesimama karibu na sadaka ya kuteketezwa pamoja na wakubwa wote wa Moabu. Balaki akamwuliza: Yawe amekuambia nini?
Yawe aniue ikiwa Saulo anakusudia kukuzuru nami nisipokujulisha kusudi uende pahali pa mbali ambapo utakuwa salama. Yawe akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.