Balamu akamwambia malaika wa Yawe: Nimetenda zambi maana sikujua kwamba umesimama katika njia kwa kunizuia. Sasa, kama haikupendezi niendelee na safari hii, basi nitarudi kwangu.
Akisi akamwita Daudi na kumwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, umekuwa mutu wa usawa. Ingekuwa jambo zuri kwangu tuende wote katika vita, kwa maana sijaona jambo baya lolote kwako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii. Hata hivyo, wakubwa hawajapendezwa nawe.
Daudi akamwambia Akisi: “Lakini nimefanya nini? Kama unavyosema kwamba haujaniona na kosa lolote tangu siku ile nilipoanza kukutumikia mpaka leo, kwa nini nisiende kupigana na waadui za bwana wangu mufalme?”