Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 29:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Akisi akamwita Daudi na kumwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, umekuwa mutu wa usawa. Ingekuwa jambo zuri kwangu tuende wote katika vita, kwa maana sijaona jambo baya lolote kwako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii. Hata hivyo, wakubwa hawajapendezwa nawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 29:6
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abramu akamwambia Sarai: “Mujakazi wako yuko chini ya mamlaka yako. Umutendee jinsi unavyopenda.” Basi, Sarai akamutesa Hagari mpaka akatoroka.


Unajua kwamba Abeneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya? Alikuja kusudi ajue mienendo yako na yale unayoyafanya.”


Lakini, ninakujua wewe Saniharibu; ninajua wakati unaikaa, wakati unatoka, na wakati unaingia; ninajua vilevile wakati kasirani yako inawaka juu yangu.


Yawe atakulinda katika shuguli zako zote tangu sasa na hata milele.


Lakini, ninakujua wewe Saniharibu; ninajua wakati unaikaa, wakati unatoka, na wakati unaingia; ninajua vilevile wakati kasirani yako inawaka juu yangu.


Basi, mwenye kujitakia baraka katika inchi, atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli. Mwenye kuapa katika inchi hii, ataapa kwa Mungu wa kweli. Maana taabu za zamani zimepita zimetoweka kabisa mbele yangu.


Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.


ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


Kuhani Finehasi na wakubwa wa jamaa za Waisraeli waliokuwa pamoja naye waliposikia maneno hayo ya watu wa makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakafurahi.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


Saulo akamwapia kwa jina la Yawe, akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi, hakuna azabu yoyote itakayokupata kutokana na jambo hili.”


Wakubwa wa waaskari wa Wafilistini waliuliza: “Waebrania hawa wanafanya nini hapa?” Akisi akawajibu wale wakubwa wa Wafilistini: “Huyu ni Daudi, mutumishi wa Saulo mufalme wa Israeli; naye amekuwa nami kwa miaka fulani. Na tangu alipokimbilia kwangu, sijamupata na kosa lolote.”


Hivyo sasa, urudi kwa nyumba. Kwenda kwa amani kusudi usiwachukize wakubwa wa Wafilistini.”


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ