Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 28:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Lakini Saulo alikataa na kusema: “Sitakula.” Lakini watumishi pamoja na yule mwanamuke, walimusihi akule, naye akawasikiliza. Kwa hiyo alisimama kutoka chini na kuikaa kwenye kitanda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 28:23
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo, Ahabu akarudi kwake akijaa chuki na huzuni nyingi, kwa sababu Naboti wa Yezereheli alimwambia kwamba hatamupa kile alichorizi kutoka kwa wazee wake. Basi, akalala kwenye kitanda, akaficha uso wake na kukataa chakula.


Siku moja Elisha alikwenda Sunemu, ambako kulikuwa mama mumoja tajiri. Mama yule akamwalika Elisha kwa chakula, na toka siku hiyo ikakuwa kawaida Elisha kula chakula kwake kila mara alipopitia kule.


Watumishi wake wakamwendea na kumwambia: “Baba yetu, kama nabii angekuambia ufanye jambo fulani gumu, haungelifanya? Sasa, aliyokuambia tu ni: ‘Ujioshe, kusudi upone!’ ”


Pahali pale kulikuwa kumepambwa kwa mapazia ya pamba ya rangi nyeupe na vitambaa vya rangi ya samawi. Mapazia hayo yalikuwa yamefungiwa pete za feza kwa kamba za kitani safi nyekundu-nyeusi, na kutundikwa kwenye nguzo za mawe ya marimari. Viti vya zahabu na feza vilikuwa vimewekwa kwenye sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi ya marimari, nyekundu, nyeusi, manjano na nyeusi.


Kumwimbia mutu mwenye huzuni ni kama kumuvua nguo wakati wa baridi, au kutia siki katika kidonda.


Kisha wakaikaa kwenye vitanda vizurivizuri, na mbele yao meza imetandikwa. Juu ya meza hiyo uliweka ubani wangu na mafuta yangu.


Halafu bwana wake akamwambia: ‘Kwenda katika njia kwenye vijiji na pembeni ya mashamba, uwalazimishe watu wafike kuingia, kusudi nyumba yangu ipate kujaa.


Lakini wakamusihi sana abakie pamoja nao, kwa maana ilikuwa magaribi na giza lilitaka kuingia. Basi akaingia ndani ya nyumba kubakia pamoja nao.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Maana upendo wa Kristo unatuongoza sisi tunaokubali kwamba ni mutu mumoja tu ndiye aliyekufa kwa ajili ya watu wote; maana yake wote wanashiriki katika kifo chake.


Sasa, unisikilize mimi mutumishi wako. Nitakutayarishia mukate kusudi ukule nawe utakuwa na nguvu za kuendelea na safari yako.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ