Basi, nabii akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Umemwachilia akuponyoke mutu ambaye niliamuru auawe. Basi, maisha yake utalipa kwa maisha yako, na watu wake kwa watu wako.’ ”
Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Tangu leo Yawe ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atamupa mutu mwingine kati ya wajirani zako anayekuwa bora kuliko wewe.
Lakini Saulo na watu wake hawakumwua Agagi, kondoo bora kabisa, ngombe wazuri, wana-ngombe, wana-kondoo na chochote kile kilichokuwa kizuri hawakukiangamiza. Lakini vitu vyote vibaya na visivyokuwa vya bei kali waliviangamiza.