13 Mufalme Saulo akamwambia: “Usiogope! Unaona nini?” Yule mwanamuke akamujibu: “Ninaona mungu akipanda toka ndani ya udongo.”
Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.
Haruni ataongea na Waisraeli kwa ajili yako. Yeye atakuwa musemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.
Yule mwanamuke alipomwona Samweli akalalamika kwa sauti kubwa, akamwambia Saulo: “Kwa nini umenidanganya? Wewe ni Saulo!”
Saulo akamwambia yule mwanamuke: “Ni mufano wa nani?” Yule mwanamuke akamwambia: “Mwanaume muzee anapanda juu, naye anajifunika kanzu.” Halafu, Saulo akatambua kwamba yule ni Samweli. Saulo akainama uso mpaka chini, kwa heshima.